Wednesday, 26 February 2014
SOMO: MALANGO/MILANGO YA KUZIMU.
MWL. EV. & PT. SONGWA .MM. KAZI – TAG – KONGOWE FOREST P.O. BOX 70983 DAR ES SALAAM.
Simu: 0757 – 567899/0789– 567899/0719 – 968160/0779 – 597066.
Email: songwak@yahoo.com. ptrsongwak@gmail.com
Maandiko ya somo: Mathayo 16:13 – 19
YALIYOMO:
1. Utangulizi.
2. Maana ya mlango.
3. Kazi ya mlango.
4. Mgawanyo wa mlango katika sura Majeshi katika ulimwengu wa Roho.
5. Kazi ya jeshi lolote.
6. Mambo yanayofungua malango ya kuzimu dhidi ya kanisa.
7. Njia ya kuyadhibiti haya malango ya kuzimu.
1. UTANGULIZI:
v Je, unayajua malango/milango ya kuzimu na kuzimu yenyewe? Kumbuka, ufahamu sahihi juu ya jambo lolote unalofanya au unalokabiliana nalo ni wa muhimu sana ili kufanikiwa vizuri.
v Acha kufanya kitu bila kuwa na ufahamu juu yake, au usipigane vita bila kujua adui yako vizuri; uwezo wake, silaha zake, mbinu zake na mawasilianao yake; lasivyo utaumia na kushindwa siku zote.
Kumbuka: Ufahamu hapa umelinganishwa na mwamba (Rock).
v Kwa nini Yesu alisema vita ya Kanisa ni dhidi ya milango ya kuzimu na siyo shetani? Fuatana nami katika somo hili.
2. MAANA YA MLANGO.
v Kwa mkutadha huu, mlango anaweza kuwa mtu au kitu chochote. Ila kwa somo hili mlango hapa ni mtu. Mfano: Adamu wa kwanza alikuwa mlango wa dhambi kuingia duniani na kuleta mauti kwa kila mwanadamu (Rumi 5:12) Adamu wa pili Yesu amekuwa mlango wa wokovu na uzima wa milele kwa kila amwaminie Yhn 10:7 – 10.
Kumbuka: Mungu hawezi kufanya jambo lolote duniani bila kupata mlango hali kadhalika hata shetani hivyo hivyo.
v Tazama mwanzo 18:17 habari za Ibrahim Kutoka 32:11, habari ya Musa, pia tazamaa Lk 22:3-6 habari yuda aliingiwa na roho ya shetani na kumsaliti Yesu. Ili shetani aingie ndani yako anahitaji mfano kumb. 28:7
3. KAZI YA MLANGO.
Kazi kubwa ya mlango ni kupitisha (kuingiza) na kutoa vitu.
Swali je, Mimi kama mlango naingiza nini na kutoa nini katika Kanisa/huduma/idara/familia/jamii?
Je, unapitisha (unaingiza) na kutoa mambo mema/mazuri katika Kanisa lako? Hapo ndipo utaelewa wewe ni lango la Mungu (Yesu) au la kuzimu kwani watu humchora shetani kuwa anasura mbaya anatisha, elewa leo kuwa shetani hayuko kama vile anavyochorwa, kwani hakuna ambaye angekubali kuwa na jitu linalotisha, wangemkimbia, hivyo shetani yuko vizuri, anasura nzuri ila kazi na matokeo yake ni mabaya sana na inatisha.
Kumbuka:
Wewe kama ni mchonganishi, mgomvi mwenye wivu, mwenye fitina na hila na tabia nyingi nyingine zinafanana nahizo zinawakilisha ufalme wa kuzimu (giza). Pia tunaposema Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo tunamaanisha haya (hawa) ni malango ya Mungu duniani yaliyopitisha vitu vizuri Tazama. Mwz. 18:17, (Ibrahim) Kutoka 32:11 (Musa).
Tazama Yoabu alikuwa mlango wa magonjwa katika ukoo wake 2Sam. 3: 27 – 29 Math. 12:43 – 45.
4. MGAWANYIKO WA MALANGO YA KUZIMU KATIKA SURA YA MAJESHI KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.
Kama unavyona majeshi ya kawaida katika nchi ndivyo katika ulimwengu wa roho adui nae anajipanga vizuri tazama Efeso 6:12 katika kila nchi kuna jeshi la:-
a) Anga Dan. 10:12 - Wanajipanga kuzuia majibu.
b) Nchi kavu Kut. 22:18 - Wachawi, waganga n.k.
c) Baharini Mk. 4:34 -5:1 – Mapepo/Majini (Kuleta) Vurugu/Machafuko
Math. 12:43 – 45
Kumbuka: Kazi ya jeshi kulinda (ulinzi) dhidi ya uvamizi, Hivyo kama kanisa tukilala tu adui anatumaliza, soma
Math 13:24 – 30
5. KAZI YA JESHI LOLOTE.
v Kazi/wajibu wa jeshi ni kulinda nchi ili isivamiwe na adui. Efeso 6:10 -18.
v Ni marufuku kwa mlinzi kulala, anatakiwa awe macho siku zote, kosa akilala tu adui hatafanya kosa. Math. 13:24-30
6. MAMBO YANAYOFUNGUA MALANGO NA KUYAPA MALANGO YA KUZIMU NGUVU DHIDI YA KANISA.
I} UOVU, DHAMBI NA MAKOSA (Isaya 59:1 – 4, 1 Yhn 3:4, Math 1:21 Rumi 3:23, 6:23, Rumi 8:1 –
v Uovu: Ni mavuno ya maovu ya watu wengine au tabia ya mtu kuzoelea kufanya
(kutenda) dhambi.
v Dhambi: Ni uasi, kuupinga utawala unao tawala kwa halali, 1Yhn 3:4, Isaya 14:12 – 17.
v Makosa: Ni mambo tufanyayo bila kujua ni kosa kutokujua jambo ni kosa. Lawi 5:17
II} LAANA: Mith 26:1 – 2, Gal. 3:13, Mwz. 3:17
Laana ni kuzuizi kisicho onekana na chenye nguvu kimsingi laana ni tatizo la kiroho.
Kumbuka:
Msingi wa laana ni matamko (maneno) Mith 6:2. Hivyo uwe mwangalifu sana juu ya maneno unayo:-
a) Jitamkia
b) Unayotamkia wengine
c) Unayotamkiwa na wengine.
Maneno hayo yanaweza kuwa kizuizi katika ulimwengu wa roho na hata kukukwamisha katika mambo yako.
III} MAKUHANI KUICHA KWELI YA MUNGU. (Hosea 4:6)
v Leo hii watumishi wengi wanalighoshi (wanaongeza maji, chumvi) na kulilazimisha neno kusema lisivyopaswa kusemwa ili kukidhi mahitaji na matamanio ya moyo wao. (personal latest) tazama 1Petro 2:1 – 5.
IV} MFUMO MBAYA WA IBADA (KUABUDU): Math 10:8
v Mfano maombi ya fedha, mbaya zaidi yanatolewa kwa kulingana na kiwango cha fedha. Hii mimi nasema biashara haramu madhababuni.
v Viongozi (makuhani husika) pamoja na wanaopewa huduma hiyo wote ni wahuni ni malango ya kuzimu kwa ajili ya kulidhofisha Kanisa la Mungu, lakini habari njema ni kwamba Mwalimu na Bwana Yesu alikwisha tangulia kusema kuwa hakuna milango ya kuzimu itakayoweza kulishinda Kanisa lake.
v Bila kulisahau wimbi kubwa la waimbaji wa nyimbo za injili; ukiangalia kwa undani ni kama wao na wachungaji wao wanakubaliana wafanye biashara ili pengine wagawane baada ya huduma husika kuisha. Nijambo la kusikitisha sana kuona mtumishi anatanguliza pesa mbele huduma baadae, hakuna fedha, hakuna huduma (lipa kwanza, upate huduma) imeshakuwa kana kwamba hizo pesa waliziwekeza, hii ni roho ya ushetani (kuzimu) hayupo Mungu hapo, hata kama kinachoimbwa kinamsema na kumtaja Mungu.
v Mbaya zaidi hata wakifanya uzinduzi matamasha ya sifa na kuabudu uzinduzi wa kazi (CD, DVD) zao ni vituko na vioja tupu. Mimi nakumbuka vizuri, Mungu alipotupa watoto tulikwenda Kanisani na sadaka ya shukrani mbele za Mungu kwa kutupa uzao (zawadi ya Mtoto), sivyo Kanisa litupe sisi sadaka ya shukrani. Sasa leo ni kinyume baada ya waimbaji hawa kutoa sadaka hiyo ya shukrani, kuonyesha shetani amepofusha hata makuhani (viongozi – wachungaji) wanaweka viingilio tena kwa madaraja na viti maalumu, huu ni utapeli na wizi wa kiroho, hata kama ulikuwa hujui leo fahamu hivyo kuwa hivyo ndivyo ilivyo na hivyo ndinyo unavyotambuliwa na Mungu. Biblia inasema siku ya mwisho wengi watalia sana wakieleza walichokifanya kwa jina la Yesu, naye Yesu atawajibu na kuwaambia tokeni hapa ninyi mbuzi siwajui Math 25:11 – 46.
USHAURI WANGU: Naelewa mnayo mahitaji mbalimbali waeleze watu mbona watakuchangia kuliko kuwaibia kwa jina la Yesu, eti kwa kisingizio cha gharama za kurekodi studio, hivi mpendwa hata haya/aibu huna, wakati ulipoenda studio ulituaga kuwa tutakulipa?, sisi sote mwajiri wetu ni Mungu. Nenda kahudumu bila kutazamia malipo na Mungu aonaye sirini atakujaza na utashangaa, kwani Mungu anajishughulisha sana na mambo yetu 1Petro 5:7.
V} USINGIZI WA KIROHO: Math 13:24 – 30
Kuwa mzembe na mzito juu ya mambo ya Mungu (Ibada) humpa adui nafasi (Efo 4:27) ya kupanda magugu mipaka (mambo tusiyoyahitaji) maishani mwetu.
VI} KUZOELEA MAMBO YA MUNGU: Amuzi 16 – 20, 2Pet 1:9
Hali ya kuwa mwenyeji na mjuzi na kuonyesha kuridhika na kutosheka na kile ulicho nacho, hivyo ukajiona unaweza kufanya chochote bila kuulizwa. Rejea kwa rafiki yetu Samsoni matokeo ya roho ya mazoea ni:-
Ø Upofu wa kiroho
Ø Uziwi wa kiroho
Ø Mfungwa wa kiroho
Ø Mtumwa wa koroho
VII} UGOMVI (MIGOGORO) KATI YA NDUGU NA NDUGU NDANI YA NYUMBA YA MUNGU (KANISANI) Kut 2:11 – 14.
v Umewahi kujiuliza, msemo huu (methali hii) isemayo fahali wawili wagombanapo au vita vya Panzi furaha kwa Kunguru.
v Ndivyo ilivyo shetani akishapata nafasi maishani mwetu anapanda mbegu magugu ya magomvi. Hivyo tunapigana sisi kwa sisi yeye humrahisishia sana kazi kutumaliza kiulaini kabisa. Ni sawa na swala wanapo pigana porini simba hatapata wakati mgumu au kazi/shida kumkamata mmoja wapo.
VIII} IBADA YA MIUNGU: Lk 10:38 – 42, Mark 4:19 Kutoka 20:4, ya Yer 17:5 – 8.
Mfano: Sanamu, watu, shughuki nyingi.
Kumbuka: Mtu au kitu chochote kinachochukua nafasi ya Mungu kinaitwa sanamu au Mungu. Hivyo uwe makini sana usije ukawa mlango wa kuzimu na kudhofisha kazi ya Mungu.
IX} WIZI WA FUNGU LA KUMI: Mal 3:8 – 11, Zek 5:1-
v Elewa kuwa wizi ni tabia ya shetani soma Yoh 10:10. Hivyo uwe mwangalifu usije ukaingia kwenye mtego wa kumwibia Mungu. Maana usipotoa fungu la kumi vita hivyo hupigani na shetani utakuwa unapambana moja kwa moja na Mungu, na hakuna aliyeshindana na Mungu akashinda. Badilika kisha chukua hatua, Amen.
7. NJIA YA KUYADHIBITI MALANGO YA KUZIMU.
I} KUWA NA UFAHAMU SAHIHI WA KWELI YA MUNGU
Yhn 8:31 – 37, Josh 7:14, Mith 11:9;21:16
Bila yakuwa na ufahamu sahihi wa neno la Mungu itakuwa ni vigumu sana kuyajua malango utaendelea kuteseka, mpaka utakapogundua lango gani limefunguliwa, kumbuka mchawi wa kwanza ya huduma/maisha yako ni wewe mwenyewe, hivyo kabla ya kumtafuta aliyesababisha tatizo jiulize wewe mwenyewe unamchango gani katika tatizo hilo. Yesu katika huduma yake hakufanya jambo bila ya kujua nini chanzo cha tatizo hilo Math 9:32 – 33.
II} KUSAMEHE (FORGIVENESS) NA KUOMBA MSAMAHA. Math 5:7, 6:9 – 14 Mark 11:25
v Hii ni njia pekee yenye nguvu kummaliza adui katika maisha yako unapokosea omba msamaha na unapokosewa samehe ni eneo tata sana na gumu kibinadamu lakini kwa ajili ya usalama na kuwekwa huru hakuna namna lazima nijifunze kusamehe kwa gharama zozote.
v Ipo hivi, japo wewe ndiyo umekosewa na ungetegemea aliyekukosea aje akuombe msamaha lakini haoni haja ya kufanya hivyo ana roho ya kifarisayo (kiburi) cha kujihesabia haki, sasa wewe kwa kuwa ndiye unayeumia kwa kitendo au vitendo anavyo/alivyo kufanyia mfano matusi, dhuluma, usengenyaji, uongo, uzushi kachukua vitu vyako. Unachopaswa kufanya ni kusamehe. Bila kufanya hivyo ni sawa na kukoroga sumu na kuinywa mwenyewe na itakudhuru peke yako, mwenzako anakula maisha.
v Kumbuka: msingi wa mimi kusamehewa na Mungu ni kuwasamehe wengine walio nikosea. Hivyo msamaha wangu umeshikiliwa na Mungu atauachia tu pale nitakapo mwachia huyu aliyenikosea. Mark 11:25.
v Elewa kwamba unaposamehe unafungua mlango wa Mungu kukupigania na kukurejeshea haki zako.
III} KUOMBA TOBA NA REHEMA.
Lawi 16:1-, Ebr 4:16, Yk 4:17, Yhn 3:21 – 22, Mith 3:3 – 4
Maombi ya toba yanarejesha ushirika uliopotea na maombi ya rehema yanashughulika na msingi wa maisha yako kuruhusu neema ya Mungu kukutetea.
Matokeo ya toba na maombi ya rehema.
a) Kibali.
b) Ujasiri.
c) Akili nzuri (ufahamu).
Kumbuka: Dhambi/uovu/makosa huondoa ujasiri wa kwenda mbele za Mungu, ila toba ya kweli na maombi ya rehema yanarejesha ujasiri na kibali.
Ukimalizana na Mungu, sasa unauwezo wa kumshughulikia adui, lakini usithubutu kumpiga shetani wakati wewe na Mungu maadui utaumia.
IV} VAA SILAHA ZOTE ZA MUNGU.
Ef 6:10 – 18, Kol 3:16, Lk 44: 1- 8, 1Kor 2:10 - , 1Yh 2:20
v Unavaa silaha zote za Mungu tayari kwa vita ya kuyashughulikia hayo malango ya kuzimu.
v Jitambue/jifahamu kuwa wewe ni mfalme/mtawala na neno la mfalme lina Nguvu yaani neno lake ndiyo sheria, ndiyo katiba, halipingwi Mh. 8:4.
Kumbuka: Kujaa i} Neno Kol 3:16
ii} Roho Mtakatifu 1Kor 2:10 – 14
UISHI MILELE.
2Kor 13:14
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment