Wednesday, 26 February 2014

IBADA YA KWELI [THE TRUE WORSHIP]




TAG – KONGOWE FOREST P.O. BOX 70983 DAR ES SALAAM.


GLORY TO GLORY CENTRE – GGC – DAR.


Mwl: Mwinj. & Mch. Songwa .M. Kazi


SIMU: 0757 – 567899/ 0789 – 567899/ 0719 – 968160/ 0779 – 597066


Email: songwak@yahoo.com/ptrsongwak@gmail.com





MAANDIKO YA SOMO: Yohana 4:20 – 24





YALIYOMO:
Maana ya Ibada.
Aina za Ibada.
Misingi 2 ya Ibada inayokubalika.
Jinsi ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli.
Matokeo ya Ibada inayokubalika.
Sura [picha] ya Ibada inayokubalika.
Maandalizi ya Ibada inayokubalika.
Tofauti kati ya Ibada na Huduma.
Sifa za jumla za Mwabudu.
Msingi wa Ibada ya kweli [Inayokubalika].





Je, umewahi kujiuliza kwa nini unakuja Kanisani?


Leo watu wengi Makanisani hawaji kuabudu bali wanakuja kupokea – kutimiza haja zao tu.


Maana ya Ibada:
Ni heshima inayotolewa na Bwana mkubwa kwa lengo la kumfanya ajisikie vizuri.



Neno Ibada siyo takatifu, ila Yule unayemfanyia Ibada ndiye ataamua Ibada yako ni ya namna gani – yaani ni takatifu [(safi) au ovu chafu)]




Ibada ni kuanguka chini ya miguu ya Bwana na kumbusu miguu au mikono [Proskuneo – Kigiriki].



Tazama. Math 15:24 – 27, Yh 5:5 – 8, 9:6 – 7, 2Falme 5:1-19 n.k.





Ibada ni utii:


Ibada ni sadaka. [kutoa] Mdo 20:35b [Heri kutoa kuliko kupokea]


Ibada ikiwa kama sadaka inalenga maeneo makuu matatu yakutoa:-
Kujitoa mwenyewe [giving yourself] Rumi 12:1.
Kutoa mambo yaujazayo moyo [heart attitudes] 1Sam 1:9 – 15, 1kor 6:19.
Kutoa mali zako [your possession] kumb. 8:18. Jua kuwa wewe na vyote ulivyonavyo sio mali yako ni ya Mungu huna cha kujivunia.





Kumbuka: Mungu hakufanya na hatafanya muujiza kwako/kwangu kama hatutaonyesha roho ya utii (Ibada) kushuka chini ya miguu yake.


Kumbuka: Mungu ni Roho, hivyo inatupasa kumwabudu katika Roho na Kweli.


Kumbuka: Msingi wa utoaji (sadaka); Mungu haangilii ulichotoa anaangali ulichokibakisha. Soma Marko 12:41 – 44 na


Luka 21:1 – 4.





1. KUMWABUDU MUNGU: Yhn 4:23


Kuna aina kuu mbili (2) za Ibada:


i) Ibada inayokubalika mbele za Mungu


ii) Ibada isiyokubalika mbele za Mungu.





I} IBADA INAYOKUBALIKA MBELE ZA MUNGU


Misingi mikuu miwili (2) ya Ibada inayokubalika ni:-


a) Kumwabudu Mungu katika Roho – 23


b) Kumwabudu Mungu katika kweli - 23





Maelezo ya:-


a} Kumwabudu Mungu katika Roho – 23
Hii ni Ibada inayotoka ndani kwenda nje na siyo nje kwenda ndani.
Haiangaalii mazingira wala hali, shauku yake Mungu kwanza apokee sifa – haki yake kasha baadaye mambo binafsi, hivyo hapa Mungu ndiyo kipaumbele. Mdo 16:25.
Ibada hii inaongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya Mwamini. Tazama Rumi 1:9 -15; Zab 103:1; 51:15 - 17





Kumbuka:


Kama moyo wako hauko sawa Ibada yako haitakubalika mbele za Mungu. Na kama Ibada ni sadaka, basi sadaka yoyote iliyo bora lazima itoke kwa Mungu.





Mfano: Isaka alitoka kwa Mungu - Mwz 16:15-19, 22:1-2, 9, 19, Yesu alitoka Mungu Yhn 3:16 na Filipi 2:5 - 11





Hivyo basi Ibada inayoongozwa na Roho Mtakatifu itakuwa sadaka itokayo kwa Mungu mwenyewe maana Roho Mtakatifu ni Mungu mwenyewe. Yoh 4:24





Jinsi ya kumwabudu Mungu katika Roho (Method of Worship).


Njia pekee ya kumwabudu Mungu katika Roho ni:-


i) Kujaa Roho Mtakatifu na kumpa nafasi ya kuyatawala/kuyaongoza maisha yako yote. Rumi 8:14, Kor2:11 - 12, 12:13





ii) Kuelekeza mawazo yako yote kwa Mungu (Thoughts centered to God).


Ni ile hali ya kuweka fahamu na akili zako zote juu ya jambo moja. Zab 22:4, Kol 3:2.





iii) Kugundua na kutafakari juu ya Neno la Mungu (Meditating God’s Word)


Kutafakari ni ile hali ya kuweka mawazo yako yote juu ya kitu/jambo moja tu.


Hivyo, kutafakari juu ya Mungu unahitaji zaidi kuwa na Muda wa kutosha wa Kuomba na kusoma Neno. 1Kor 2:10,


Luka 10:38 - 42, Zab 27:4





Hivyo ili kupata ufunuo wa Neno la Mungu, unahitaji kuwa na ushirika wa karibu sana na Roho Mtakatifu.


2Kor 13:14, 1Kor 2:10 - 13.





b} Kumwabudu Mungu katika Kweli - 23


Hiii ni Ibada ambayo misingi yake imejengwa kwatika Neno la Mungu na siyo hisia na msukumo wa nje. (mbwembwe) zingine kama ujanja na uongo. Zab. 119:160, 142; 2kor 4:2, Rumi 1:18 - 19, 25, Yhn. 18:37 - 38; 17:17 - 18, Zab47:7





Kumbuka:


Usichanganye kweli ya Mungu na uongo (uovu).





Matokeo ya Ibada inayokubalika:


i) Mungu anatukuzwa - Zab. 50:23


ii) Waumini wanasafishwa - Zab. 24:3 - 4


iii) Kanisa linajengwa - Mdo. 5:28


iv) Waliopotea wanahubiriwa Injili. 1Kor. 14:23 - 25





Sura ya picha ya Ibada inayokubalika:


Ni manukato/harufu nzuri mbele ya Mungu. Kutoka 30:34 - 38, Yhn. 12: 3 - 8





Maandalizi ya Ibada inayokubalika mbele za Mungu:


Anza na maombi ya Rehema na utakaso mbele za Mungu ili upatane na Mungu ili unapokwenda mbele zake asione kitu kisicho safi (kichafu) akageuka na kukuacha. Kumb. 23:14
Tazama. Ebr 4:10 - 16, 10:19 - 22, Mithali. 3:3 - 4, 1Yhb. 3:21, Yak. 4:7, Zab 24:3-5, Lawi 16:1 -





Tofauti kati ya Ibada na Huduma:


Kuna tofauti kubwa kati ya Huduma na Ibada, kwa kifupi ni kwamba;-


Ibada ni ile inayotoka chini (kwetu) kwenda juu kwa (Mungu) kwa nguvu za Roho Mtakatifu kupitia njia ya Yesu wakati Huduma ni ile itokayo juu kwa (Mungu) kuja chini (kwetu) kwa njia ya Yesu na kwa nguvu za Roho Mtakatifu katika mfumo na karama za rohoni.


1Kor. 12:1 - 11





Hivyo Mungu atashuka kuhudumu yaani kukutana na mahitaji yetu pale tu atakapo kuwa ameipokea ibada yetu (amefurahishwa na ibada yetu).





Kumbuka:
Tatizo kubwa leo wakristo tupo kihuduma zaidi na siyo kiibada; tunaweza kufananisha na (kizazi cha Matha Luka 10:38-48).



Tunapaswa kujifunza kwa Mariam Zab 27:4 na Luka 10:38-42



Kwa hiyo fanya chochote uwezacho kufanya kitakacho mfanya Mungu ajisikie vizuri, maana sahau kupokea kitu kutoka kwa Mungu - BWANA kama Ibada yako haijamfurahisha.





Mungu tangu zamani alishuka kuhudumu, kuchukua au kupokea sadaka n.k. baada ya kupendezwa na ibada hiyo.


Sasa tafuta cha kufanya katika nyumba ya Mungu kitakachompelekea Mungu ajisikie vizuri na kukubariki na kukutendea mambo makuu ya kushangaza. Tazama Mwanzo 4:4 - Sadaka ya Habili.











II} IBADA ISIYOKUBALIKA MBELE ZA MUNGU.
Zifuatazo ni baadhi ya Ibada ambazo Mungu hazipokei kamwe japo walengwa watoa mbele za Mungu wa kweli Mpendwa ni jambo la kuogofya na kusikitisha sana kwenda mbele za Mungu kumwabudu kisha Ibada yako ikakataliwa. Rejea habari za wana wa Adam Habili na Kaini - Mwanzo 4:1-15.



Jambo linalotokea kwa mwamini pale Ibada inapokataliwa ni kuwa roho/moyo wenye chuki (Hatred), wivu (Jelous), kuhukumu (Judgementalism) na uchungu (bitterness) kwa wale wanafanikiwa, barikiwa, kuinuliwa kutumiwa na Mungu n.k.




Usiumize kichwa wala usipate shida na watu kama hao juwa tatizo lao ni kiwango/kimo chao cha Ibada mbele za Mungu bado kipo chini sana ya kiwango na hivyo usipambane nao kimwili washauri wainue viwango vyao vya ibada kwa kuomba, kusoma Neno la kushiriki katika ratiba za Ibada za Kanisa na huduma mbalimbali za kiroho.






Kumbuka:


Watu wengi wagomvi, wachochezi, wezi wa mafungu ya kumi, wasiotulia makanisani (wachanga wa kiroho) wanaosusa kufanya huduma hao wote viwango vyao vya Ibada na Ufahamu wa kweli ya Mungu viko chini ya kiwango. Malaki 3:8-11, Malaki 2:1-4, Zekaria 5:1-4.





ZIFUATAZO NI BAADHI TU YA IBADA ZISIZOKUBALIKA MBELE ZA MUNGU.





a} Ibada itolewayo kwa Miungu. (The Worship of False of God).


Miungu ni vitu vinavyochukua nafasi ya Mungu vyaweza kuwa mali, wazazi, shughuli n.k. (vitu vya dunia - Earhtly materials na sanamu za mfano wa vitu vya mbinguni - Heavenly things) na kumfanya Mungu kuwa wa baadaye. Kutoka 34:14 - Bwana ni Mungu mwenye wivu, Ayubu 31:24-28 usikwke tumaini kwenye vitu na Yoshua 24:20, Kumb 4:14-19, Mark 4:19.





b} Ibada itolewayo kwa Mungu wa kweli katika njia/mfumo mbaya. (The Worship of the true God in a wrong form).


Kutoka 32:1-28 Haruni - wana Israel na ndama ya kuyeyusha.


Mungu hatapokea Ibada itolewayo kwa miungu ya uongo hatapokea ibada itolewayo kwake kwa mfumo mbaya.





c} Ibada itolewayo kwa Mungu wa kweli kwa namna au kwa mtazamo wa mtu apendavyo yeye. ( The Worship of the


true God in a self - styled manners).



Hii ni roho ya mazoea - ilimtesa Samson - Amuni 16:20-21. Mdo 5:1-11 Anania na Safira hii ni kumshusha/kumpunguza Mungu na kumweka katika kiwango cha miungu.




Walawi 10:1-20 watoto wa Haruni, Nadadu na Abihu walikufa kwa sababu walitoa dhabihu wakiwa wamelewa mbele za Mungu tazama Lawi 10:9.




1Samweli 13:8-14 Habari za Mfalme Saul alipoingilia majukumu ya Nabii, Kuhani na Mwamuzi Samweli - ufalme wake haukudumu. 2Nyakati 26:16-21.




Habari Uza aliyekufa baada ya kulinyonyeshea mkono sanduku la Agano. 2Sam 6:1-9.




Habari ya Mafarisayo na Waandishi walivyokuwa wanafiki - Mnafiki ni rafiki adui. Math 15:1-9;23:23-28 (katika zaka na maombi).






d} Ibada itolewayo kwa Mungu wa kweli katika nia mbaya. (The Worship of the God with a wrong attitude)
Nia ni namna mtu anavyofikiria au mtu anavyohisi au ona kuhusu mtu mwingine.





Kumbuka:
Kama tukiabudu hali mioyo na hisia zetu haziko sawa au sahihi hiyo haitakubaliwa na Mungu.



Tazama mfano wa sadaka vipofu na vilema zilitolewa.

Malaki 1:6-14, 3:13-15, 4:1-6, Amos 5:21-22, Hosea 6:4-7, Isa 1:11-20, Mark 7:6





Kumbuka:
kiwango changu cha Ibada ndicho kitakacho amua hatima yangu uko vile ulivyo kwa sababu ya kiwango chako cha ibada.



Matatizo mengi leo hata kwenye ndoa ni kwa sababu viwango vya ibada viko chini. Hebu jaribu leo Mama/Baba, kumuheshimu au kumfurahisha mmeo/mkeo utashangaa tatizo lililodumu kwa miaka nenda rudi linatoweka bila hata kufunga na kuomba au kuombewa. Kol 3:18-19 na Efeso 5:22-29.




Hata mtoto ukiinua kiwango chako cha Ibada utashangaa namna utakavyopata kibali mbele ya wazazi wako. Kol 3:20. Pia hata vijana wengi kutokupata/kutokuoa au kuoelewa leo makanisani, ukifuatilia sana kiwango chao cha Ibada kipo chini, hebu kijana - askari wa Kristo nenda kaongeze kiwango chako cha Ibada utashangaa utakavyoa anza kutafutwa kila mtu atatamani kuwa karibu yako. Rejea kwa Yesu, popote alipo kwenda watu walimtafuta na kumfuata. Soma Luka 21:38 na kitabu cha Marko.






Kumbuka:
Tuliumbwa na kuokolewa kwa ajili ya Ibada - kumwabudu Mungu na kumtumikia.
Ebrania 12;28, Rumi 12:1, Efeso 1:3, Kutoka 10:24-29, Uf. 22:3.





Sifa za jumla za mwabudu - mtoa Ibada wa Kiroho na Kweli (True Worshiper).
Awe na imani juu ya Mungu. Hebr 11:6.




Aisha maisha mtakatifu (maisha safi) Zab 24:3-4, 1Kor 3;16, Math 5:8.






Kumbuka:
Msingi wa Ibada ya kweli inayokubalika ni USAFI. Zab 24:3-4 na Yoh 4;23.





Mungu akubariki kwa kusoma somo hili nina imani kuwa limebadilisha maisha yako nakuinua kiwango chako cha Ibada. Basi kama hivyo ndivyo; wasidie na wengine kuzijua kweli hizi ili tulijenge kanisa la Kristo. Kumbuka kupata maarifa na ujuzi na kisha usiutekeleze/kuutendea kazi huko sio kujifunza. Yak. 1:22 na Math 7:24-27








Uishi Milele


2Kor 13:14







No comments:

Post a Comment