Mwl: Mwinj & Mch. SONGWA, MM. KAZI
MAANDIKO: Ebr 4:16, Mith 3: 3 – 4, 1 Yhn 3:21-22.YALIYOMO:
1. Utangulizi
2. Maana ya Rehema na Neema
3. Kazi ya Maombi ya Rehema na matokeo yake
4. Faida ya Maombi ya Rehema
5. Aina ya msaada upatikanao kwa Neema kwa njia ya Maombi ya Rehema
01. UTANGULIZI
Je, umewahi kukaa chini na kujiuliza maana ya maneno haya mawili maarufu sana; yaani Rehema na Neema?
Je, unajua Rehema hushughulika hasa na nini katika maisha ya mwamini? Hali kadhalika na Neema hushughulika na mambo gani katika maisha ya mwamini?
Basi; kwa kuifahamu zaidi fuatana nami katika somo hili. Na Mungu akubariki sana.
02. MAANA YA REHEMA NA NEEMA
I. REHEMA:
- Ni ile hali ya kutopata adhabu unayostahili kabisa kupewa kwa sababu ya uovu, dhambi au makosa yaliyofanywa nyuma.
- Ni msamaha wa mwisho wa Mungu uambatanao na kusitishwa kwa adhabu stahiki
- Ni kutopata unachostahili
- Ni msamaha
KUMBUKA: Kimsingi Maombi ya Rehema ni Toba ya kweli mbele za Mungu dhidi ya uovu, dhambi na makosa yaliyofanyika nyuma, Kut 20: 1 -4.
II. NEEMA:
- Ni kupewa usichostahili
- Ni hali kustahilishwa, kupendezwa, kuhurumiwa na Mungu (Favour and Spiritual Blessings of the Lord Jesus Christ.)
- Kuhesabiwa haki vure ( kazi ya msalaba)
03. KAZI YA MAOMBI YA REHEMA NA MATOKEO YAKE
I. Kazi ya maombi ya Rehema;
(a) Kufuta hati ya mashitaka; hali ya kuondoa uhalali wa shetani kututawala na kukutumikisha, Kol. 2 : 14
Pindi unaporudi kwa Yesu unapewa haki na uweza Yhn 1;12
(b) Kupata Ujasiri mbale za Mungu 1 Yhn 3: 21- 22, Mwanzo 3: 8 – 19.
Tabia za Mtu jasiri
Josh 1:1-9, Sam 17: 8-47, Amuzi 14:6, 19, 15:4, 13, 15, 16:3, 27
- Hana hofu ( Fearless person)
- Ana uhakika, anajiamini, shupavu, ana matumaini ( confident person)
- Ni shujaa, thabiti, jeuri (bold person)
-
Mambo yanayoondoa ujasiri ni; Isaya 59: 1-4
- Uovu, dhambi na makosa yetu.
Kumbuka: Kitu pekee kinachompa kiburi na jeuri shetani cha kututesa na kututawala ni ni uovu, dhambi na makosa yasiyotubiwa, Yhn 8: 34, 42-44
Hivyo Mungu anakusihi utubu ili akurejeshee ujasiri na mamlaka ya kumshinda aduui, Ezek 18: 21- 23.
(c ) Kutupa Kibali mbele za: Mith 3: 3- 4, Lk 2 : 52
- Mungu – Ushirika mzuri na Mungu
- Wanadamu – kusikilizwa, kutambuliwa, kufurahishwa na kuheshimiwa.
Kumbuka:
Mtu anapoteza kibali mbele za Mungu na wanadamu; katika ulimwengu wa roho anakuwa kama mtu aliyepakwa mavi usoni na anatoa harufu chafu ( uvundo). Hata kama mtu ana huduma nzuri , ana karama na vipawa vizuri akipoteza kibali tu, hatakubalika kamwe mpaka atengeneze na Mungu, Malaki 2:3.
Angalizo:
Uwe makini kulinda kibaki- ushirika mzuri na Mungu na wanadamu ili usije ukapakwa mavi usoni – ukapoteza kibali.
(d) Kutupa akili nzuri mbele za ; Mith 3:3-5, 24: 3-9, 1 Kor 15: 33- 34
- Mungu
- Wanadamu
Biblia inasema sana juu ya akili, kuwa Mungu ameruhusu tuzitumie akili lakini siyo kuzitegemea kwani akili zina mwisho wake.
Matunda ya akili nzuri ni; Mith 24: 3-6, 3: 13-20
- Hekima (nguvu), maarifa (elimu).
- Ufahamu (Ujuzi na ustadi)
Kumbuka: Urithi wa mwenye akili ni maarifa kwani ana busara, bali urithi wa mjinga (asiye na akili) ni upumbavu, Mith 14: 18
Jambo la msingi la kuelewa vizuri kati ya Rehema na Neema ni kwamba;
-Rehema kazi yake ni kushughulikia MSINGI wa maisha ya mtu, Zab 11:3, yaani mambo ya nyuma. Yanawezekana mengine huyakumbuki; haya ni pamoja na yote yaliyotendwa na watu wengine pamoja na yale uliyotenda mwenyewe.
-Mambo ya nyuma yana uwezo wa kukukwamisha mbele ya safari hata usiweze kuumaliza mwendo; yaani kuyatimiza malengo na makusudi ya Mungu katika maisha yako.
-Neema kazi yake ni kushughulikia JENGO (Maisha) – 1Kor 3:9- 15, na mambo yajayo Ebr 4: 16 (Tazama pia Yer 1:10, Math 13: 24-30, Math 15:13_)
04. FAIDA YA KUMWENDEA MUNGU KWA MAOMBI YA REHEMA
Ebr 4: 16 na Math 5: 7
Faida ni matunda mazuri ya kitu au jambo.
Zifuatazo ni baadhi ya faida:
(i) Tunapokea Rehema ( Msamaha) kwa yale tuliyoshindwa ( Help for our failures)
(ii) Tunapata Neema ya kutusaidia katika nyakati ngumu za uhitaji, 2 Kor 12 : 9- 10)
05. AINA YA MSAADA UPATIKANAO KWA NEEMA KWA NJIA YA MAOMBI YA REHEMA
Ebr 4: 16
Tunapata:
(i) Msaada ufaao ( appropriate help)
(ii) Msaada ujao kwa muda/ majira/ wakati sahihi kabisa wa Mungu ( Divine well-timed help)
Kumbuka: Toba ya kweli huleta Ufalme wa Mungu kwenye maisha ya mtu, Math 4 :17, 3: 2
UISHI MILELE
2Kor 13;14
IMEANDALIWA NA:
Mwl: Mwinj & Mch. SONGWA, MM. KAZI
SIMU: 0757-567899. 0789-567899. 0719-968160, 0779-597066
Email: songwa@yahoo.com ptrsongwak@gmail.com
TAG KONGOWE FOREST. DSM. P.O. Box 70983. DSM.
No comments:
Post a Comment